Zijue Aina Tano Za Chabo Vyuoni
Wanangu wa ram ndogoo hii inatuhusu yanii. Kama ulikuwa hujui chuo kutoboa sio lelemama kuna mbinu nyingi za kivita zinahitajika , kama sio mtu wa kukamia sanaaa wewe basi ndio mwanetu yani chabo boi au chabo gal. Leo nakuletea njia tano zinazo tumika kupiga chabo vyuoni, kaa kwa kutulia twende sambamba.
Njia ya Kwanza: Chabo Kengeza
Chabo hii ni ya kibabe yani, unatazama kama hutazami vile. Oya wee hii ni pale ume kaa na mwana mkamiaji anatiririka majibu kwenye pepa kinachobakia ni kengeza moja lina nasa majibu matatu, hapo ni unatkiwa kumasta tu engo za kengeza zuri. Unaachaje kutumia njia hii kwa mfano
Njia ya pili: Chabo Msusio
Hii ni babkubwa, utake nini sasa. Nipale mwamba anapoamua kukupa pepa zima ukopi na kupesti tu kazi ni kwako, sasa hii tunaiita lulu imedondoka kwenye giza.
Njia ya Tatu: Chabo darubini
Hapa unapaswa uwe na uwezo mkubwa wa kuona mbali yaani uwe mlaji wa karoti sana. Ukipiga jicho umbali wa mita mbili hadi tatu uwe na uwezo wa kuisoma karatasi ya mkamiajii na kuyanyaka majibu chapu, hii ni ya wachache wewee. Kama unajijua unachangamoto za kuona mbali hii haikuhusu.
Njia ya Nne: Chabo nipasie
Hii inahitaji uwe na kiungo msambambazaji , ni pale ambapo mpo watatu alafu kati kuna mtu mwingine ambaye anachukua majibu kutoka kwa mkamiaji na kukupa wewe, kwa hii njia jamaa wakatikati anatakiwa awe fundi sana yani maana akifeli tu lazima uyavagae.
Njia ya Tano: Chabo Ishara
Ni pale kushika sikio , kuashika pua, kuonesha idadi ya vidole nakadhalika huwa na maana. Aisee hii njia ni salama na bora zaidi kulinganisha na zote zilizoelezwa hapo juu.
Je wewe unatumia ipi kati ya hizo mwanangu?


Comments (0)
No Comments
Write a Comment